Wadau wangu wooote ninawapa hi! hii blog ni yetu wote leta mada watu tuijadili na atakayejifanya yeye namna gani vipi anataka kuvuruga amani tunamuashia moto sisi sote ni vijana na tunachangamoto nzito si kwenye mapenzi, uchumi, majirani feki,na mambo kibao sasa huu ndio uwanja wetu kila alikuwa na dukuduku na aseme tumshauri...WEWE NA MIMI NI KITU KIMOJA.... karibuni saaanaaaaa
TUZUNGUMZE CO.LTD
Masuala yote ya kijamii,mapenzi,uchumi,siasa,michezo,matukio nk utayapata kupitia blog hii
Wednesday 23 October 2013
Monday 18 March 2013
Njia rahisi ya kupata mtaji wa kuanzisha biashara
Heshima kwenu wadau,
Kibiashara kuna njia nyingi za kupata mtaji wa biashara hasa kwa zile zinazoanza ingawa nyingi kati ya hizo ni NGUMU sana, hivyo kupelekea watu wengi kuwa na mawazo mazuri ya kibiashara lakini hushindwa kuyafanikisha kutokana na mitaji. Kwa mtazamo wangu, naona kama ukitumia njia ya kuomba fedha kidogo kidogo kutoka kwa watu wengi walio karibu yako, wanaokuamini, kukuheshimu, kukufahamu na wenye uwezo kiasi itakuwa njia rahisi ukilinganisha na mikopo kutoka taasisi za kifedha ambapo utajikuta unafanya biashara kwa presha na hofu ya kurejesha deni. unaweza kufanya kama ifuatavyo kwa kuchukulia uhitaji wa mtaji wa Tsh 10,000,000:
1 - kuomba / kuazima / kukopa Tsh 100,000 kutoka kwa watu 100 = Tsh 10,000,000
2 - kuomba / kuazima / kukopa Tsh 200,000 kutoka kwa watu 50 = Tsh 10,000,000
3 - kuomba / kuazima / kukopa Tsh 350,000 kutoka kwa watu 30 = Tsh 10,000,000
4 - kuomba / kuazima / kukopa Tsh 500,000 kutoka kwa watu 20 = Tsh 10,000,000
5 - kuomba / kuazima / kukopa Tsh 1,000,000 kutoka kwa watu 10 = Tsh 10,000,000
NB: - Naamini tunafahamiana na watu wengi sana tangu mtoto unakua hadi hapo ulipo, kuanzia uliocheza nao, marafiki wa primary, sekondary, vyuo, kazini, majirani, ndugu, jamaa, marafiki, marafiki uliojuana nao kwenye mitandao kama JF, Facebook, Twitter nk..nina hakika hutakosa watu wasiopungua 100 wenye nia, uelewa na uwezo wa kukufanikishia hili.
- Uhitaji, madhumuni ya kuomba, muda wa kurejesha, malengo ya matumizi inategemea na makubaliano yako na unayemuomba, na si lazima hao watu utakao waomba wajue kusudio lako la njia hii ya kupata mtaji, pia usiombe kama msaada, omba kama mkopo ili baada ya muda mfupi kama miezi miwili ama mitatu uahidi kurejesha.
- Nina imani kiasi cha Tsh 10,000,000 ni mtaji tosha kwa biashara ndogo ndogo kwa kuanzia. Mfano: jiko la baa, kibanda cha chips, salon ya kiume, stationary, internet cafe, duka la jumla, duka la kawaida, genge, grecery, bajaji, duka la nguo hasa mitumba bomba nk.. ambapo itakuwa rahisi kwako kwa muda wa miezi mitatu kuweza kurejesha fedha ulizoomba.
Je, wajua njia/mbinu za kutangaza biashara yako?
Waswahili wanasema, kizuri kula na mwenzio.
Natumai
maarifa haya yatawafaa wengi wenu ambao mnafikiria kuanzisha biashara au
mlio na biashara pia, mnahitaji kujua njia/ mbinu za kutangaza
biashara zenu.
1.Jitambulishe/Watambulishe
wengine- Wenzetu katika lugha ya Kiingereza wanaita kitu hiki
“networking”. Kwa bahati mbaya, Kiswahili hakina neno mbadala la moja kwa moja
kuhusu “networking” hii. Kwa kifupi, ni kwamba ukiwa na biashara, kila
unayekutana naye anaweza kuwa mteja wako.Jitambulishe bila aibu.Mjue na yeye
akujue, mwambie unachokifanya(biashara yako).Pia usisahau marafiki zako.Je
marafiki zako wanajua unachokifanya? Watu wengi huwa wanasahau kwamba marafiki
wanaweza kuwa chanzo kizuri sana cha mauzo au kuongezeka kwa idadi ya
wateja.Waambie marafiki zako na wao(hususani kama ni marafiki kweli) bila shaka
watawaambia marafiki zao pia.
1.Kuwa
na tovuti (website)- Katika zama za leo,ni muhimu kwa biashara kuwa na
tovuti. Natambua kwamba sio biashara zote zinaweza au zina uwezo wa kuwa na
tovuti. Unachotakiwa hapa ni wewe mwenyewe kujiuliza, je aina hii ya biashara
niliyonayo inahitaji uwepo wa mtandaoni kupitia tovuti? Ni swali na jibu ambalo
wewe mwenyewe sharti ulipatie majibu. Uzuri wa tovuti au uwepo wa mtandaoni ni
kwamba hata pale biashara yako inapokuwa imefungwa(usiku kwa mfano kwa biashara
za mchana) bado unakuwa unaendelea kuitangaza.
1.Mitandao
Jamii Ni Lazima- Sidhani kama natakiwa kusisitiza zaidi jinsi gani ni
muhimu kutangaza huduma au bidhaa zako kupitia mitandao jamii kama vile Blogs,
Facebook,Twitter,LinkedIn,Google Plus etc. Kama unapenda kuandika,kwa mfano,
anzisha blog.Andika,weka video za huduma unazozitoa.Siku hizi kamera nyingi
zina uwezo wa kuchukua video.Kwanini usijichukue video ya dakika mbili
ukielezea bidhaa au huduma unazozitoa na kutuma mtandaoni kupitia mitandao
jamii? Bila shaka marafiki zako watakupata vizuri zaidi na wao wanawapelekea
wengine video hiyo.Ujumbe utaenea.
1.Orodhesha
Biashara Yako katika Huduma Za Orodha Za Biashara-
Hatua muhimu katika biashara ni kutambulika. Njia mojawapo nzuri ya kuchukua au
kufikia hatua hii ni pamoja na kujiorodhesha. Kwa mfano,biashara yako
inahusiana na mazao ya kilimo.Kama kuna umoja/ushirikiano wa wafanyabiashara wa
mazao ya kilimo hakikisha kwamba jina lako na la biashara yako yanakuwepo
katika orodha hiyo. Pia katika nchi mbalimbali zipo huduma za kujiorodhesha
zinazoitwa Kurasa Za Njano(Yellow Pages). Hakikisha kwamba biashara yako ipo
ndani. Pia search engines kama vile Google,Yelp,Yahoo,Bing nk zinazo huduma
mbalimbali za kuorodhesha biashara mbalimbali katika nchi. Itumie fursa hiyo.
Angalizo: Katika kujiorodhesha kuwa makini,zipo huduma za Bure na Za
Kulipia.Kazi Ni Kwako.
1.Tumia
Barua Pepe Kutangaza/Kujitangaza-Siku hizi watu wengi wana
e-mail address(anuani pepe). Bila shaka hata wewe msomaji unayo.Kwanini basi
usiitumie hiyo anuani pepe kuwasiliana na wateja wako?Anapokuja kwenye sehemu
yako ya biashara,muombe mteja anuani pepe yake ili panapokuwa na “deal”
umtumie.Mara nyingi hakuna atakayekataa. Kila mtu anapenda “deal”.Ukishakuwa na
anuani pepe,kwanini usimkumbuke mteja wako aidha kwa “deal” au kumtumia e-card
ya X-mas,Eid nk? Angalizo: Usiwatumie wateja wako mambo mengi mengi mara
kwa mara.Wanaweza dhani ni spammers na hivyo waka-block kabisa barua
pepe kutoka kwako.
1.Gawa
Business Cards- Niliwahi kusikia kisa cha jamaa fulani ambaye
alitengeneza business cards nzuri sana. Alipoona ni nzuri sana akagoma
kuzigawa.Akawa anaenda nazo kwenye mikutano nk lakini hazigawi.Unajua
kilichotokea? Biashara ikafa akabaki na business cards zake.Nnachotaka kusema
ni kwamba kila fursa inapojitokeza,gawa business cards zako.Na usigawe tu na
kutosema kitu.Mwambie kwa maneno machache yule unayempatia business card kuhusu
biashara yako. Muombe na yeye akupe business card yake kama anayo. Kwa maneno
mengine ukifanya hili unakuwa pia umefanya lile nililolizungumzia mwanzoni
kabisa.
1.Shiriki
Katika Huduma/Shughuli za Kijamii- Kama mfanyabiashara,njia
mojawapo rahisi ya kuifanya jamii ikutambue ni pamoja na kushiriki katika
shughuli mbalimbali zinazoendelea katika jamii. Unaweza kushiriki kama mdhamini
au mfanyakazi wa kujitolea. Mara nyingi huduma/shughuli hizi za kijamii huwa
zinahudhuriwa na watu wa habari(media) na kwa maana hiyo unaweza kuwa umepata
“matangazo bila kulipia”. Lakini cha muhimu zaidi ni kwamba unaposhiriki katika
shughuli za kijamii ni ishara kwamba unaijali jamii hiyo. Unapofanya hivyo ni
rahisi na wewe kuungwa mkono na wana jamii hao.
1.Muombe
Mtu(mwandishi,blogger,mtangazaji nk) afanyie mapitio(review) bidhaa yako-
Utaratibu huu bado haujaingia sana nchini kwetu.Lakini mimi binafsi naukubali
sana. Kama unauza bidhaa fulani na unaamini kwamba bidhaa yako ni
bora,utafaidika sana endapo mtu kama mwandishi,blogger,mtangazaji wa
televisheni,radio nk,atakapoitumia bidhaa yako,kuona matokeo yake na kisha
kwenda hewani na kuwaambia wanaomsikiliza kuhusu bidhaa aliyoitumia. Naomba
nisisitize hapa kwamba ni muhimu akawa ameitumia kweli na kupata matokeo
anayoyapigia debe.Kinyume chake ni kwamba yeye ataharibu heshima yake na wewe
utakuwa umekosa lundo kubwa zaidi la wateja. Angalizo: Kuna waandishi au
bloggers na watangazaji nk ambao hawafanyi mapitio BURE..Ongea nao muelewane.
1.Hudhuria
na Tumia Vizuri Maonyesho Ya Biashara/Mikutano-Sio
kila biashara inaweza kushiriki katika maonyesho ya biashara hususani yale
makubwa kama vile Saba Saba au Nane Nane.Lakini yapo maonyesho mengine
mbalimbali(mfano kupitia wizara za serikali au umoja fulani wa
wafanyabiashara). Kila inapowezekana,usilaze damu.Shiriki.Pia shiriki mikutano mbalimbali
inayoandaliwa kwa ajili ya wafanyabiashara fulani. Kwa uzoefu wangu,mikutano ya
aina hii ipo na inafanyika mara kadhaa tena bila malipo.Shiriki.Unapokwenda
huko beba kadi zako za biashara,vipeperushi nk.Gawa,ongea na wenzako,toa
mchango na mawazo yako.
1.Tangaza
Kwenye Magazeti,Televisheni,Radio,Blogs Nk: -Miongoni mwa
njia/mbinu zote nilizozitaja hapo juu,pengine hii ndio ikawa ya gharama zaidi.
Lakini ukweli ni kwamba matangazo,yanalipa kwa maana ya kwamba,kama uwezo
upo,basi angalia uwezekano wa kutangaza kupitia njia hizi. Lakini kitu kimoja
ambacho ni vizuri kukizingatia hapa ni kwamba unapoamua kutangaza kupitia njia
hizi,kuwa mbunifu.Usifanye tu kile ambacho washindani wako wa kibiashara
wanafanya. Jaribu kuwa na mawazo huru na binafsi. Pasua kichwa,fikiri.
10 Steps to Starting a Business ( njia 10 za kuanzisha biashara ndogo)
Starting
a business involves planning, making key financial decisions and
completing a series of legal activities. These 10 easy steps can help
you plan, prepare and manage your business. Click on the links to learn
more.
Step 1: Write a Business Plan
Use these tools and resources to create a business plan. This written guide will help you map out how you will start and run your business successfully.Step 2: Get Business Assistance and Training
Take advantage of free training and counseling services, from preparing a business plan and securing financing, to expanding or relocating a business.Step 3: Choose a Business Location
Get advice on how to select a customer-friendly location and comply with zoning laws.Step 4: Finance Your Business
Find government backed loans, venture capital and research grants to help you get started.Step 5: Determine the Legal Structure of Your Business
Decide which form of ownership is best for you: sole proprietorship, partnership, Limited Liability Company (LLC), corporation, S corporation, nonprofit or cooperative.Step 6: Register a Business Name ("Doing Business As")
Register your business name with your state government.Step 7: Get a Tax Identification Number
Learn which tax identification number you'll need to obtain from the IRS and your state revenue agency.Step 8: Register for State and Local Taxes
Register with your state to obtain a tax identification number, workers' compensation, unemployment and disability insurance.Step 9: Obtain Business Licenses and Permits
Get a list of federal, state and local licenses and permits required for your business.Step 10: Understand Employer Responsibilities
Learn the legal steps you need to take to hire employees.
Subscribe to:
Posts (Atom)